Menejimenti ya Shirika la Nyumba wakiwa kwenye Kikao cha Kamati ya Baraza la Wawakilishi ya kuchunguza na kudhibiti hesabu za Serikali za Mitaa na Mashirika ya umma katika kuwasilisha majibu ya Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali kwa Mwaka wa fedha 2020/2021 kilichofanyika tarehe 11/11/2022 Makao Makuu ya Shirika yaliopo Darajani, Zanzibar. Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika pamoja na Uongozi wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar.